Noble Quran » Swahili » Sorah Al-Bayyinah ( The Clear Evidence )
Choose the reader
Swahili
Sorah Al-Bayyinah ( The Clear Evidence ) - Verses Number 8
لَمْ يَكُنِ الَّذِينَ كَفَرُوا مِنْ أَهْلِ الْكِتَابِ وَالْمُشْرِكِينَ مُنفَكِّينَ حَتَّىٰ تَأْتِيَهُمُ الْبَيِّنَةُ ( 1 )
![Al-Bayyinah ( The Clear Evidence ) - Ayaa 1](style/default/icons/mp3.png)
Hawakuwa walio kufuru miongoni mwa Watu wa Kitabu na washirikina waache walio nayo mpaka iwajie bayana,
رَسُولٌ مِّنَ اللَّهِ يَتْلُو صُحُفًا مُّطَهَّرَةً ( 2 )
![Al-Bayyinah ( The Clear Evidence ) - Ayaa 2](style/default/icons/mp3.png)
Yaani Mtume aliye toka kwa Mwenyezi Mungu anaye wasomea kurasa zilizo takasika,
وَمَا تَفَرَّقَ الَّذِينَ أُوتُوا الْكِتَابَ إِلَّا مِن بَعْدِ مَا جَاءَتْهُمُ الْبَيِّنَةُ ( 4 )
![Al-Bayyinah ( The Clear Evidence ) - Ayaa 4](style/default/icons/mp3.png)
Wala hawakufarikiana walio pewa Kitabu ila baada ya kuwajia hiyo bayana.
وَمَا أُمِرُوا إِلَّا لِيَعْبُدُوا اللَّهَ مُخْلِصِينَ لَهُ الدِّينَ حُنَفَاءَ وَيُقِيمُوا الصَّلَاةَ وَيُؤْتُوا الزَّكَاةَ ۚ وَذَٰلِكَ دِينُ الْقَيِّمَةِ ( 5 )
![Al-Bayyinah ( The Clear Evidence ) - Ayaa 5](style/default/icons/mp3.png)
Nao hawakuamrishwa kitu ila wamuabudu Mwenyezi Mungu kwa kumtakasia Dini, wawe waongofu, na washike Sala, na watoe Zaka. Na hiyo ndiyo Dini madhubuti.
إِنَّ الَّذِينَ كَفَرُوا مِنْ أَهْلِ الْكِتَابِ وَالْمُشْرِكِينَ فِي نَارِ جَهَنَّمَ خَالِدِينَ فِيهَا ۚ أُولَٰئِكَ هُمْ شَرُّ الْبَرِيَّةِ ( 6 )
![Al-Bayyinah ( The Clear Evidence ) - Ayaa 6](style/default/icons/mp3.png)
Hakika walio kufuru miongoni mwa Watu wa Kitabu na washirikina wataingia katika Moto wa Jahannamu wadumu milele humo. Hao ndio viumbe waovu kabisa.
إِنَّ الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ أُولَٰئِكَ هُمْ خَيْرُ الْبَرِيَّةِ ( 7 )
![Al-Bayyinah ( The Clear Evidence ) - Ayaa 7](style/default/icons/mp3.png)
Hakika walio amini na wakatenda mema, hao ndio bora wa viumbe.
جَزَاؤُهُمْ عِندَ رَبِّهِمْ جَنَّاتُ عَدْنٍ تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ خَالِدِينَ فِيهَا أَبَدًا ۖ رَّضِيَ اللَّهُ عَنْهُمْ وَرَضُوا عَنْهُ ۚ ذَٰلِكَ لِمَنْ خَشِيَ رَبَّهُ ( 8 )
![Al-Bayyinah ( The Clear Evidence ) - Ayaa 8](style/default/icons/mp3.png)
Malipo yao kwa Mola wao Mlezi ni Bustani za daima, zipitazo mito kati yake. Wakae humo milele. Mwenyezi Mungu yu radhi nao, na wao waradhi naye. Hayo ni kwa anaye mwogopa Mola wake Mlezi.
Random Books
- KAULI YA QURAN NA KAULI ZA AHLI BAIT WA MTUME SAW KUHUSIANA VIPENZI VYA ALLAH-
Source : http://www.islamhouse.com/p/336325
- MASWALI 60 KWA WAKRISTOMASWALI 60 KWA WAKRISTO.
Source : http://www.islamhouse.com/p/371266
- KAULI YA QURAN NA KAULI ZA AHLI BAIT WA MTUME SAW KUHUSIANA VIPENZI VYA ALLAH-
Source : http://www.islamhouse.com/p/336325
- UJUMBE WA UISLAMU KWA ULIMWENGU MZIMA-
Source : http://www.islamhouse.com/p/385737
- KAULI YA QURAN NA KAULI ZA AHLI BAIT WA MTUME SAW KUHUSIANA VIPENZI VYA ALLAH-
Source : http://www.islamhouse.com/p/336325