Noble Quran » Swahili » Sorah Al-Muzzammil (The One wrapped in Garments)
Choose the reader
Swahili
Sorah Al-Muzzammil (The One wrapped in Garments) - Verses Number 20
أَوْ زِدْ عَلَيْهِ وَرَتِّلِ الْقُرْآنَ تَرْتِيلًا ( 4 )
![Al-Muzzammil (The One wrapped in Garments) - Ayaa 4](style/default/icons/mp3.png)
Au izidishe - na soma Qur'ani kwa utaratibu na utungo.
إِنَّ نَاشِئَةَ اللَّيْلِ هِيَ أَشَدُّ وَطْئًا وَأَقْوَمُ قِيلًا ( 6 )
![Al-Muzzammil (The One wrapped in Garments) - Ayaa 6](style/default/icons/mp3.png)
Hakika kuamka usiku kunawafikiana zaidi na moyo, na maneno yake yanatua zaidi.
وَاذْكُرِ اسْمَ رَبِّكَ وَتَبَتَّلْ إِلَيْهِ تَبْتِيلًا ( 8 )
![Al-Muzzammil (The One wrapped in Garments) - Ayaa 8](style/default/icons/mp3.png)
Na lidhukuru jina la Mola wako Mlezi, na ujitolee kwake kwa ukamilifu.
رَّبُّ الْمَشْرِقِ وَالْمَغْرِبِ لَا إِلَٰهَ إِلَّا هُوَ فَاتَّخِذْهُ وَكِيلًا ( 9 )
![Al-Muzzammil (The One wrapped in Garments) - Ayaa 9](style/default/icons/mp3.png)
Mola Mlezi wa mashariki na magharibi, hapana mungu isipo kuwa Yeye, basi mfanye kuwa Mtegemewa wako.
وَاصْبِرْ عَلَىٰ مَا يَقُولُونَ وَاهْجُرْهُمْ هَجْرًا جَمِيلًا ( 10 )
![Al-Muzzammil (The One wrapped in Garments) - Ayaa 10](style/default/icons/mp3.png)
Na vumilia hayo wayasemayo, na jitenge nao kwa vizuri.
وَذَرْنِي وَالْمُكَذِّبِينَ أُولِي النَّعْمَةِ وَمَهِّلْهُمْ قَلِيلًا ( 11 )
![Al-Muzzammil (The One wrapped in Garments) - Ayaa 11](style/default/icons/mp3.png)
Na niache Mimi na hao wanao kanusha, walio neemeka; na wape muhula kidogo!
إِنَّ لَدَيْنَا أَنكَالًا وَجَحِيمًا ( 12 )
![Al-Muzzammil (The One wrapped in Garments) - Ayaa 12](style/default/icons/mp3.png)
Hakika Sisi tunazo pingu nzito na Moto unao waka kwa ukali kabisa!
وَطَعَامًا ذَا غُصَّةٍ وَعَذَابًا أَلِيمًا ( 13 )
![Al-Muzzammil (The One wrapped in Garments) - Ayaa 13](style/default/icons/mp3.png)
Na chakula kinacho kwama kooni, na adhabu inayo umiza.
يَوْمَ تَرْجُفُ الْأَرْضُ وَالْجِبَالُ وَكَانَتِ الْجِبَالُ كَثِيبًا مَّهِيلًا ( 14 )
![Al-Muzzammil (The One wrapped in Garments) - Ayaa 14](style/default/icons/mp3.png)
Siku ambayo ardhi itatikiswa na milima pia, na milima itakuwa kama tifutifu la mchanga!
إِنَّا أَرْسَلْنَا إِلَيْكُمْ رَسُولًا شَاهِدًا عَلَيْكُمْ كَمَا أَرْسَلْنَا إِلَىٰ فِرْعَوْنَ رَسُولًا ( 15 )
![Al-Muzzammil (The One wrapped in Garments) - Ayaa 15](style/default/icons/mp3.png)
Hakika Sisi tumemtuma kwenu Mtume aliye shahidi juu yenu, kama tulivyo mtuma Mtume kwa Firauni.
فَعَصَىٰ فِرْعَوْنُ الرَّسُولَ فَأَخَذْنَاهُ أَخْذًا وَبِيلًا ( 16 )
![Al-Muzzammil (The One wrapped in Garments) - Ayaa 16](style/default/icons/mp3.png)
Lakini Firauni alimuasi huyo Mtume, basi tukamshika mshiko wa mateso.
فَكَيْفَ تَتَّقُونَ إِن كَفَرْتُمْ يَوْمًا يَجْعَلُ الْوِلْدَانَ شِيبًا ( 17 )
![Al-Muzzammil (The One wrapped in Garments) - Ayaa 17](style/default/icons/mp3.png)
Basi nyinyi mkikufuru, mtawezaje kujikinga na Siku ambayo itawafanya watoto wadogo waote mvi?
السَّمَاءُ مُنفَطِرٌ بِهِ ۚ كَانَ وَعْدُهُ مَفْعُولًا ( 18 )
![Al-Muzzammil (The One wrapped in Garments) - Ayaa 18](style/default/icons/mp3.png)
Hapo mbingu zitapasuka! Ahadi yake itakuwa imetekelezwa.
إِنَّ هَٰذِهِ تَذْكِرَةٌ ۖ فَمَن شَاءَ اتَّخَذَ إِلَىٰ رَبِّهِ سَبِيلًا ( 19 )
![Al-Muzzammil (The One wrapped in Garments) - Ayaa 19](style/default/icons/mp3.png)
Kwa hakika hili ni kumbusho. Mwenye kutaka atashika njia ya kwendea kwa Mola wake Mlezi.
إِنَّ رَبَّكَ يَعْلَمُ أَنَّكَ تَقُومُ أَدْنَىٰ مِن ثُلُثَيِ اللَّيْلِ وَنِصْفَهُ وَثُلُثَهُ وَطَائِفَةٌ مِّنَ الَّذِينَ مَعَكَ ۚ وَاللَّهُ يُقَدِّرُ اللَّيْلَ وَالنَّهَارَ ۚ عَلِمَ أَن لَّن تُحْصُوهُ فَتَابَ عَلَيْكُمْ ۖ فَاقْرَءُوا مَا تَيَسَّرَ مِنَ الْقُرْآنِ ۚ عَلِمَ أَن سَيَكُونُ مِنكُم مَّرْضَىٰ ۙ وَآخَرُونَ يَضْرِبُونَ فِي الْأَرْضِ يَبْتَغُونَ مِن فَضْلِ اللَّهِ ۙ وَآخَرُونَ يُقَاتِلُونَ فِي سَبِيلِ اللَّهِ ۖ فَاقْرَءُوا مَا تَيَسَّرَ مِنْهُ ۚ وَأَقِيمُوا الصَّلَاةَ وَآتُوا الزَّكَاةَ وَأَقْرِضُوا اللَّهَ قَرْضًا حَسَنًا ۚ وَمَا تُقَدِّمُوا لِأَنفُسِكُم مِّنْ خَيْرٍ تَجِدُوهُ عِندَ اللَّهِ هُوَ خَيْرًا وَأَعْظَمَ أَجْرًا ۚ وَاسْتَغْفِرُوا اللَّهَ ۖ إِنَّ اللَّهَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ ( 20 )
![Al-Muzzammil (The One wrapped in Garments) - Ayaa 20](style/default/icons/mp3.png)
Hakika Mola wako Mlezi anajua ya kuwa hakika wewe unakesha karibu na thuluthi mbili za usiku, na nusu yake, na thuluthi yake. Na baadhi ya watu walio pamoja nawe kadhaalika. Na Mwenyezi Mungu ndiye anaye ukadiria usiku na mchana. Anajua kuwa hamwezi kuweka hisabu, basi amekusameheni. Basi someni kilicho chepesi katika Qur'ani. Anajua ya kuwa baadhi yenu watakuwa wagonjwa, na wengine wanasafiri katika ardhi wakitafuta fadhila ya Mwenyezi Mungu, na wengine wanapigana katika Njia ya Mwenyezi Mungu. Kwa hivyo someni kilicho chepesi humo, na mshike Sala, na toeni Zaka, na mkopesheni Mwenyezi Mungu mkopo mwema. Na kheri yoyote mnayo itanguliza kwa ajili ya nafsi zenu mtaikuta kwa Mwenyezi Mungu, imekuwa bora zaidi, na ina thawabu kubwa sana. Na mtakeni msamaha Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe Mwenye kurehemu.
Random Books
- Wanawake katika Uislamu Ukilinganisha na Wanawake katika Mafundisho ya Kiyahudi-Kikristo-
Source : http://www.islamhouse.com/p/191551
- KUSAFISHA KUW AAMINI UCHAFU WA KUTO AMINI-
Source : http://www.islamhouse.com/p/339834
- Vipi tusome Tarekhe ya Aal-Beit na Masahaba?-
Source : http://www.islamhouse.com/p/336327
- Maswali YaliyowaongozaVijana wa Kishia Kuingia Katika HakiMaswali YaliyowaongozaVijana wa Kishia Kuingia Katika Haki.
Source : http://www.islamhouse.com/p/369244
- Wanawake katika Uislamu Ukilinganisha na Wanawake katika Mafundisho ya Kiyahudi-Kikristo-
Source : http://www.islamhouse.com/p/191551